Mbuzi, Mbwa na Ng'ombe (Paka rangi)
Brigid Simiyu
Marleen Visser
Kiswahili


Mbuzi, Mbwa na Ng'ombe walikuwa marafiki wakubwa.
Siku moja walisafiri kwa teksi.
Siku moja walisafiri kwa teksi.
Walifika mwisho wa safari yao.
Dereva aliwauliza walipe nauli zao.
Ng'ombe akalipa.
Dereva aliwauliza walipe nauli zao.
Ng'ombe akalipa.
Mbwa hakuwa na kiasi kamili cha pesa, akalipa zaidi kidogo.
Dereva alikuwa anajitayarisha kumrudhishia Mbwa baki ya pesa zake.
Wakati huo, Mbuzi alitoroka bila kulipa chochote.
Wakati huo, Mbuzi alitoroka bila kulipa chochote.
Dereva akakasirika sana.
Akaondosha gari bila kumrudishia Mbwa baki ya pesa zake.
Akaondosha gari bila kumrudishia Mbwa baki ya pesa zake.
Hiyo ndiyo sababu, siku zote, Mbwa hulikimbilia gari.
Nia yake ni kumpata dereva amrudishie baki ya pesa zake.
Nia yake ni kumpata dereva amrudishie baki ya pesa zake.
Mbuzi, anapousikia mlio wa gari, hutoroka.
Yeye huogopa kushikwa kwa kukosa kulipa nauli.
Yeye huogopa kushikwa kwa kukosa kulipa nauli.
Ng'ombe huwa hashughuliki gari linapokuja.
Yeye huchukua muda kuvuka barabara.
Anajua kwamba alilipa nauli yake kamili!
Yeye huchukua muda kuvuka barabara.
Anajua kwamba alilipa nauli yake kamili!
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Mbuzi, Mbwa na Ng'ombe (Paka rangi)
Author - Fabian Wakholi
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Marleen Visser
Language - Kiswahili
Level - First sentences
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Marleen Visser
Language - Kiswahili
Level - First sentences
© African Storybook Initiative 2014
Creative Commons: Attribution 4.0
Source www.africanstorybook.org
Creative Commons: Attribution 4.0
Source www.africanstorybook.org

