Paka mwerevu
Ursula Nafula
Catherine Groenewald

Bwana Kio anaishi kijijini kwetu.

Ana paka anayeitwa Safi.

1

Bwana Kio anapoenda kazini, anauacha mlango wazi.

2

Safi anaketi mlangoni na kuilinda nyumba.

3

Mbwa wa jirani akiikaribia nyumba, Safi anamtisha.

Yuko tayari kumkwaruza kwa kucha zake.

4

Mbwa anatoroka na kurudi kwao.

5

Jirani akiugusa malango wa nyumba, Safi anamwona.

Yuko tayari kumkwaruza.

6

Jirani anageuka haraka na kwenda zake.

7

Safi anapohisi njaa, anajua la kufanya.

Anaufunga mlango, kisha anaenda kula.

8

Safi anakula kutoka bakuli lake la bluu.

Anakipenda chakula chake sana.

9

Akimaliza, anaruka juu ya sofa na kulala.

"Purr! Purr! Purr!"

10

Bwana Kio anarudi nyumbani jioni.

Safi anajinyoosha kwa furaha na kumlaki.

11

Bwana Kio na Safi wanaketi sebuleni.

Kila mmoja anasoma gazeti.

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Paka mwerevu
Author - Ursula Nafula
Illustration - Catherine Groenewald
Language - Kiswahili
Level - First sentences