Teksi ya Nanu
Marion Drew
Marion Drew

Hujambo! Jina langu ni Nanu.

Mimi na mamangu tunasubiri teksi ili twende nyumbani.

1

Hapa nimesimama kwenye foleni.

Mamangu ananiimbia wimbo. "Njoo Bwana Teksi kwani huoni! Twasubiri, mimi na Nanu!"

2

Mwanamke aliye karibu nami anawapeleka kuku nyumbani.

Watataga mayai ili ale.

3

Wanaume hawa wanarudi kutoka kazini. Wanatabasamu.

Nawasikia wakiimba, "Nanu mdogo, usiwe na wasiwasi. Teksi yaja kwa haraka."

4

Mwanamke anapita akitembea. Yuko nadhifu sana.

Viatu vyake si vizuri kweli! Vinatoa sauti, "Click, click, click. Click, click, click," anapotembea.

5

Mwanamme huyo anauza vinywaji baridi.

Napenda vinywaji baridi. Ni baridi na vitamu sana.

Je, unavipenda?

6

Hebu! Kuna wanawake wamebeba vichwani chakula chao cha jioni.

Je, si wao ni werevu?

7

Mwanamke huyo anasukwa nywele zake.

Ataenda nje leo usiku na marafiki zake.

8

Nimechoka sasa. Mamangu ananiweka mgongoni kwake nikapumzike.

Anaimba, "Tafadhali Bwana Teksi, usichelewe. Gogo anasubiri kwenye lango kuu."

9

Kuna rafiki yangu Tumi. Yeye pia anapumzika.

Tutakuwa nyumbani hivi karibuni.

10

Hapo juu ndege wanaruka kwenda nyumbani.

Lazima wafike nyumbani kabla giza halijaingia.

11

Mwanamke huyu ana vipuli maridadi. Nadhani alivinunua mjini leo.

Nikiwa mkubwa, nitanunua vipuli vingi vyangu na vya mamangu.

12

Mamangu anaanza kuchoka sasa.

Ninamwimbia wimbo, "Tafadhali Bwana Teksi, njoo. Mimi na mamangu tunasubiri."

13

Ngoja! Ninasikia teksi!

Hii hapa inakuja!

14

Hii ni teksi yetu kubwa nyekundu.

Imekuja kunipeleka mimi na mamangu nyumbani.

Nimefurahi sana!

15

Kwaheri!

16
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Teksi ya Nanu
Author - Marion Drew
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Marion Drew
Language - Kiswahili
Level - First sentences