Sababu ya chura kuwa na sura mbaya
Mozambican folktale
Hélder de Paz Alexandre

Miaka mingi iliyopita, Mjusi na Chura walikuwa marafiki.

Siku moja waliamua kuwatafuta wasichana wapenzi jijini.

1

Chura alimwonea Mjusi wivu.

Mjusi alikuwa na ngozi iliyometameta na ya kuvutia.

2

Chura alimwuliza, "Ni kitu gani ulichofanya ukawa mrembo hivi? Hebu, nitazame, nina sura mbaya mno. Ninawezaje kuirembesha ngozi yangu?"

3

Mjusi alimjibu, "Sikiliza! Tia maji chunguni kisha ukiweke mekoni. Halafu u..."

4

Hakumaliza usemi wake. Chura alimjibu, "Ninajua tayari, najua. Fyata ulimi, rafiki yangu." Kisha aliondoka.

5

Chura alipofika nyumbani, aliyatia maji chunguni.

6

Maji yalipoanza kuchemka, alijitumbukiza ndani.

7

Ngozi yake ikachomeka na mkia wake ukakatika!

8

Na badala ya kumetameta na kuwa mrembo kama Mjusi, alikuwa na sura mbaya zaidi!

9
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Sababu ya chura kuwa na sura mbaya
Author - Mozambican folktale
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Hélder de Paz Alexandre
Language - Kiswahili
Level - First sentences