Hapo zamani, kulikuwa na panya wawili.
Mmoja wao aliishi nyikani.
Panya mwingine aliishi katika nyumba.
Siku moja, panya aliyeishi katika nyumba alimwambia panya wa nyika, "Wewe chakula chako si kizuri, usingizi wako umejaa mang'amung'amu huku mvua ikikulowesha."
"Sisi tunalala fofofo katika nyumba za watemi. Tunakula vyakula vingi mno. Siku moja nitembelee ujionee fahari iliyopo," alisema panya wa nyumba.
"Niko tayari usiku wa leo kama mrija unaosubiri kinywaji," akajibu panya wa nyika.
Wakati huo huo mwenye nyumba alikasirika ajabu akifoka matusi, "Panya hawa wanaokula chakula changu wataona cha mtema kuni!"
Ndipo akawategea mtego uliojaa sukari.
Panya waliingia nyumbani kula vitamu vilivyokuwamo.
Walikuwa wakicheka, "Chu. Chu. Chi. Chi. Che. Che!"
Walipoufikia mtego, panya wa nyumba alisema, "Wacha nionje sukari. Tazama vitamu vitamu tunavyokula hapa."
Lakini kabla panya hajapata kugusa sukari, mtego ukamnasa kichwa. Pa!
Macho yake yakabubujika kama mbilingani.
Panya wa nyika akamtazama akiwa ameduwaa.
Akasema, "Heee rafiki yangu, kitamu kipi ulichokula kikayafanya macho yabubujike?"
Lakini panya wa nyumba alishindwa kujibu.
Panya wa nyika akaondoka akikejeli, "Du! Umekula vizuri. Mimi siviwezi vitamu hivyo unavyojivunia."
Kuwepo nyumbani kulikochakaa mradi kwako, ni bora kuliko kuwepo nyumbani kuzuri sana ilhali ni nyumba ya jirani yako.