Hamisi abahatika
Adelheid Marie Bwire
Rob Owen

Siku moja Hamisi na babake walienda sokoni kununua sare ya shule.

1

Hamisi akamwona kijana mwingine amevalia shati la kijani kibichi.

"Anaonekana nadhifu sana," Hamisi aliwaza.

2

"Shati lile lapendeza sana," Hamisi alimwambia babake.

3

Hamisi aliendelea kusema, "Tafadhali baba, ninunulie shati la kijani kibichi kama hilo."

4

"Hamisi, leo nitaweza kununua sare ya shule pekee." Baba alisema.

5

"Sina pesa za ziada za kukununulia shati kama hilo." Baba akaeleza.

6

Baada ya kulipia sare, baba alitambua kuwa alikuwa na pesa zilizobaki.

Angeweza kumnunulia Hamisi shati la kijani kibichi!

7

Hamisi alifurahi sana.

Alikimbia kwenda kujichagulia shati la kijani kibichi.

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Hamisi abahatika
Author - Adelheid Marie Bwire
Illustration - Rob Owen
Language - Kiswahili
Level - First sentences