Mbuzi, Mbwa na Ng'ombe (Paka rangi)
Fabian Wakholi
Marleen Visser

Mbuzi, Mbwa na Ng'ombe walikuwa marafiki wakubwa.

Siku moja walisafiri kwa teksi.

1

Walifika mwisho wa safari yao.

Dereva aliwauliza walipe nauli zao.

Ng'ombe akalipa.

2

Mbwa hakuwa na kiasi kamili cha pesa, akalipa zaidi kidogo.

3

Dereva alikuwa anajitayarisha kumrudhishia Mbwa baki ya pesa zake.

Wakati huo, Mbuzi alitoroka bila kulipa chochote.

4

Dereva akakasirika sana.

Akaondosha gari bila kumrudishia Mbwa baki ya pesa zake.

5

Hiyo ndiyo sababu, siku zote, Mbwa hulikimbilia gari.

Nia yake ni kumpata dereva amrudishie baki ya pesa zake.

6

Mbuzi, anapousikia mlio wa gari, hutoroka.

Yeye huogopa kushikwa kwa kukosa kulipa nauli.

7

Ng'ombe huwa hashughuliki gari linapokuja.

Yeye huchukua muda kuvuka barabara.

Anajua kwamba alilipa nauli yake kamili!

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Mbuzi, Mbwa na Ng'ombe (Paka rangi)
Author - Fabian Wakholi
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Marleen Visser
Language - Kiswahili
Level - First sentences