Khayanga aliishi na wazazi wake kwa furaha.
Alipokuwa na umri wa miaka kumi, walifariki.
Khayanga alitunzwa na Rosa, mmoja wa jamaa zake.
Rosa alikuwa mkarimu lakini alikuwa mkongwe.
Khayanga aliyatembelea makaburi ya wazazi wake.
Aliwaeleza matatizo yake.
Siku moja alipokuwa makaburini, alipokea zawadi ya kibuyu.
Aliamini kuwa kilitoka kwa wazazi wake.
Khayanga aliusikia wimbo mtamu wa kuliwaza kutoka katika kibuyu.
Uliimbwa hivi:
Khayanga, ee,
Khayanga!
Mtoto wetu, mpendwa!
Kibebe kibuyu hiki, mpendwa!
Kikuliwaze, mpendwa!
Khayanga alifahamu sauti hiyo kuwa ya mamake.
Khayanga alikibeba kibuyu chake wakati wote.
Aliamini kwamba wazazi wake walimlinda.
Siku moja, kibuyu hicho kilivunjika.
Khayanga alivunjika moyo vilevile.
Alivishika vigae hivyo mikononi akaimba:
Babangu, mamangu!
Kibuyu changu kimevunjika!
Nifanyeje?
Nipe ishara nyingine!
Nijue mko nami!
Sauti ilisema:
Khayanga mtoto wetu!
Viokote vigae hivyo!
Vitumie kuchota maji!
Ioshe miguu yako!
Yafumbe macho!
Khayanga alitii.
Khayanga alikibeba kibuyu chake kila mahali. Waliomwona, walijiuliza, "Hiki ni kibuyu cha aina gani?"
Kibuyu hicho kilimsaidia kupata mahitaji yake.
Khayanga aliamini kuwa wazazi wake walikuwa naye wakati wote.
Hakuna lolote baya lingeweza kutendeka kwake.