Kuku na Jongoo walikuwa marafiki. Lakini walikuwa wakishindana kila wakati.
Siku moja waliamua kucheza kandanda ili kuona aliyekuwa mchezaji bora.
Walienda uwanjani wakaanza mchezo. Kuku alicheza kwa kasi, lakini Jongoo akacheza kwa kasi zaidi.
Kuku alipiga teke mpira ukaende mbali, lakini Jongoo aliupiga ukaenda mbali zaidi.
Kuku alianza kukasirika.
Waliamua kucheza penalti. Kwanza Jongoo alikuwa mlinda lango. Kuku alifunga bao moja tu.
Basi ikawa zamu ya Kuku kulinda lango.
Jongoo akaupiga mpira na kufunga bao. Jongoo akapiga chenga akafunga bao. Akapiga mpira wa kichwa na kufunga bao.
Jongoo alifunga mabao matano!
Kuku alikasirika kwamba alipoteza. Alikuwa mbaya sana aliposhindwa.
Jongoo alianza kucheka kwa sababu rafiki yake alikuwa anauzingatia mchezo huo sana isivyofaa.
Kuku alikasirika sana hadi akafungua mdomo wake wazi na kummeza Jongoo.
Kuku alipokuwa akienda nyumbani, alikutana na Mama Jongoo. Mama Jongoo aliuliza, "Je, umemuona mtoto wangu?"
Kuku hakusema chochote. Mama Jongoo alikuwa na wasiwasi.
Kisha Mama Jongoo akasikia sauti ndogo ikilia, "Mama, nisaidie!"
Mama Jongoo aliangalia kila mahali na kusikiliza kwa uangalifu. Sauti ilitoka ndani ya kuku.
Mama Jongoo alipiga kelele, "Tumia nguvu yako maalum mtoto wangu!"
Jongoo wanaweza kutoa harufu na ladha mbaya. Kuku alianza kuwa mgonjwa.
Kuku aliteua. Kisha alimeza na kutema. Halafu akapiga chafya na kukohoa. Akakohoa!
Ladha ya Jongoo ilichukiza!
Kuku alikohoa hadi akamtema Jongoo.
Mama Jongoo na mtoto wake walitambaa wakaenda mtini ili kujificha
Kuanzia wakati huo, kuku wote na jongoo walikuwa maadui.