Hisia huja na kwenda
Mimi Werna
Joe Werna

Ada anacheka kwa sababu alisikia hadithi ya kuchekesha.

Anatabasamu.

Ada anahisi nini?

1

Tisa anahisi hasira.

Ana mkunjo kipajini kwake.

Kwa nini amekasirika?

2

Yadoo anaogopa giza.

Kila mtu huhisi hofu wakati mwingine.

Lakini Yadoo anaweza kuomba msaada.

3

Chidu ana wasiwasi juu ya kazi yake ya shule.

Anaweza kumwambia mwalimu wake.

Anaweza kuomba msaada.

4

Lushan anacheza cheza!

Ni sawa kufanya mchezo wakati mwingine.

5

Ethuro anajisikia mwenye huzuni.

Ni sawa kulia.

Hisia huja na kwenda.

6

Yatoo amejawa na furaha.

Yeye amefurahi.

Hisia huja na kwenda.

7

Hadiza anahisi uvivu.

Anahitaji kupata kitu cha kufanya.

8

Ayoo ana hasira.

Amechanganyikiwa.

Hasira ni hisia ngumu.

9

Lizy amesisimka.

Je! Ni nini sababu ya msisimko wake?

Mama alitayarisha chakula akipendacho.

10

Zege alihisi usingizi.

Alikuwa amechoka sana.

"Lakini, 'kuhisi usingizi' ni hisia?" Effy anauliza.

11

Effy amechanganyikiwa!

Je! Unaweza kujibu swali lake?

12

Lempaa anahisi mshangao na mshtuko.

Alisikia uvumi fulani.

Ni ukweli?

13

Nelly ni mgonjwa.

Anahisi huzuni.

Anahitaji dawa na kupumzika ili ajisikie bora.

14

Selina anahisi kutosheka.

Amemaliza kazi zake za nyumbani.

Sasa anaweza kucheza.

15

Victor hana kazi leo.

Anamwonyesha Selina vidole viwili.

"Kazi nzuri, sasa hebu tucheze!" anasema.

16
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Hisia huja na kwenda
Author - Mimi Werna
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Joe Werna
Language - Kiswahili
Level - First sentences