Uamuzi (Paka rangi)
Ursula Nafula
Vusi Malindi

Mtaa wetu ulikuwa na matatizo mengi.

Tulisimama kwenye foleni tukisubiri kuchota maji kutoka mfereji mmoja.

1

Tulisubiri kupokea chakula cha msaada.

Hatukuwafahamu wahisani wetu.

2

Usalama ulizorota kila uchao.

Tulilazimika kufunga nyumba zetu mapema kwa ajili ya wizi.

3

Baadhi ya watoto waliacha shule.

Wazazi wao hawakuweza kuwalipia karo.

4

Wasichana wadogo walifanya kazi za nyumbani pale mtaani.

5

Wavulana wadogo walirandaranda ovyo.

Wengine waliwafanyia watu kazi mashambani.

6

Upepo ulivuma na kuzipeperusha karatasi chafu.

Ziliangikwa mitini na uani na kuyachafua mazingira.

7

Vipande vya chupa vilitupwa ovyo ovyo njiani.

Watu walijeruhiwa walipokatwa navyo.

8

Siku moja, mfereji wa maji ulikauka na mitungi yetu ikawa tupu.

Tulijiuliza, "Sasa tutayapata maji wapi?"

9

Babangu alitembea kutoka nyumba hadi nyumba.

Aliwatangazia watu kuhudhuria mkutano wa mtaa.

10

Watu walikusanyika chini ya mti ule ule ambako tulipokea chakula cha msaada.

Baadhi waliuliza, "Kuna nini leo?"

11

Babangu alisimama katikati yao akasema, "Lazima tuyabadilishe maisha ya mtaa wetu."

12

Juma, aliyekuwa amepanda juu ya mti, alisema kwa sauti, "Naweza kusafisha uwanja wa nyumba zetu."

13

Mwanamke mmoja wa makamo, alisema, "Sisi wanawake tutaungana pamoja tupande mbegu ili tupate chakula."

14

Mwanamume mwingine alisimama akasema, "Wanaume nao watachimba kisima cha maji."

15

Sote tulisema kwa sauti moja, "Lazima tubadilishe maisha yetu."

Hivyo ndivyo, tulianza kufanya kazi pamoja kuyabadilisha maisha yetu.

16
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Uamuzi (Paka rangi)
Author - Ursula Nafula
Adaptation - Ursula Nafula
Illustration - Vusi Malindi
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs