Fana na wanyama wake (Paka rangi)
Foziya Mohammed
Jesse Breytenbach

Fana na familia yake wanaishi katika mji wa Debre Birhan nchini Ethiopia. Fana ni mwanafunzi wa darasa la tatu. Ana roho nzuri na mwenye hekima.

1

Fana anawapenda wanyama. Ana paka mmoja, kuku wawili, mbuzi na njiwa. Anakuwa nao kwa muda mrefu akiwalisha na kucheza nao.

2

Siku moja, Fana na wenzake walikuwa wakicheza uwanjani shuleni. Fana aliwaona watoto wakiwarushia njiwa mawe.

Alijiuliza, "Mbona wanawaumiza njiwa?"

3

Aliacha kucheza akakimbia kuelekea mahali watoto wale walikokuwa.

Mwanzoni, wenzake hawakuelewa kilichokuwa kikitendeka. Walimfuata. Fana aliwakemea wale watoto, "Acheni kurusha mawe."

4

Wale watoto watukutu walitoroka.

Fana aliwashika njiwa waliojeruhiwa. Aliona majeraha kwenye mbawa zao. Aliamua kuwapeleka nyumbani kuwalinda.

5

Fana aliwalisha njiwa. Jioni aliisimulia familia yake alichokiona na kufanya siku ile na jinsi alivyowaokoa njiwa.

6

Asubuhi, Fana na wazazi wake welienda katika kliniki kupata dawa za kuwaponya njiwa.

Baada ya siku chache, njiwa walipona majeraha yao. Fana alifurahi sana.

7

Kila mara, Fana aliwaambia marafiki zake, "Ninawapenda wanyama. Wanyama wana manufaa kwetu na ni marafiki zetu. Lazima tuwalinde na kuwahifadhi."

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Fana na wanyama wake (Paka rangi)
Author - Foziya Mohammed
Adaptation - Ursula Nafula
Illustration - Jesse Breytenbach
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs