Siafu na Njiwa mvivu
Terkule Aorabee
Joe Werna

Siafu alikuwa mkulima mzuri.

Aliishi kwenye ardhi na familia yake.

1

Walifanya bidii katika shamba lao.

Familia ya Siafu iliishi vizuri.

2

Njiwa alikuwa jirani ya Siafu.

Njiwa aliishi kwenye mti na familia yake.

3

Njiwa na familia yake hawakulima.

Walistarehe mchana kutwa.

4

Njiwa na familia yake waliimba vizuri.

5

"Mtatugawia chakula?" Njiwa aliuliza.

"La! Limeni chenu!" Siafu alijibu.

6

Njiwa aliruka chini na kuanza kuimba, "Siafu ni mfalme!"

7

Walipewa chakula.

Baada ya kula, Njiwa na familia yake walirudi kwao.

8

Kesho yake, Njiwa alimkejeli Siafu.

"Kwani wafalme wana vichwa vikubwa?"

9

"Samahani!" Njiwa alisema, halafu akaanza kuimba, "Siafu ni mfalme!"

10

"Huna shukuruni. Tena wewe ni mvivu!" Siafu alilalamika.

11

"Siafu ni mfalme! Siafu ni mfalme! Siafu ni mfalme!"

Siafu alifurahi.

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Siafu na Njiwa mvivu
Author - Terkule Aorabee
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Joe Werna
Language - Kiswahili
Level - First words