Kulisubiri basi
Mecelin Kakoro
Mango Tree

Sam yuko tayari kwenda mjini leo asubuhi.

"Basi linatarajiwa kufika saa 3 asubuhi," mama anatabasamu.

Sam yuko tayari masaa mawili kabla basi kuwasili.

1

Sam na mamake wanawasili kwenye kituo cha basi saa 2:45 asubuhi.

2

Watu zaidi walikuja kwenye kituo kabla ya 3 asubuhi.

Nusu saa baadaye, bado wamesubiri.

3

Sam ana wasiwasi. "Labda basi limeharibika," anawaza.

"Labda hatutakwenda mjini leo. Labda sitapata sare zangu za shule."

4

Saa 3:45 asubuhi baadhi ya watu wanakata tamaa na kurudi nyumbani.

Sam anaanza kulia. "Tutasubiri kidogo zaidi," mama anamtuliza.

5

Ghafla, wanasikia kelele.

Basi linakuja!

6

Basi linawasili kituoni saa 4 kamili za asubuhi.

7

"Ingieni! Ingieni! Tumechelewa sana leo!" dereva anasema.

8

Abiria wanaingia na kuketi.

Basi linaondoka saa 4:10 asubuhi.

9

"Basi litaondoka mjini saa ngapi kurudi kijijini?" mamake Sam anauliza.

"Basi la bluu litaondoka mjini saa 8:30 alasiri," dereva anajibu.

10

Sam anawaza, "Tutawasili mjini saa 5 kamili mchana."

"Tutakuwa na muda kiasi gani mjini kabla basi kuondoka?" Sam anaendelea kuwaza.

11

Maswali zaidi kuhusiana na hadithi:
1. Sam alikuwa tayari kwenda mjini saa ngapi?
2. Sam na mamake walisubiri basi kwa muda gani?
3. Basi lilichelewa kwa dakika ngapi?
4. Safari kwenda mjini itachukuwa dakika ngapi?
5. Sam na mamake watafika kijijini saa ngapi ikiwa basi la bluu linaondoka mjini kwa wakati?

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Kulisubiri basi
Author - Mecelin Kakoro
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Mango Tree
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs