Paka na Mbwa na Yai
Elke and René Leisink
Elke and René Leisink

Huyu ni Paka.

Huyu ni Mbwa.

1

Paka na Mbwa wanatembea.

Wanatembea kijijini kwao.

2

Kisha wanaliona yai.

Yai liko nyasini.

Yai liko peke yake nyasini.

Yai liko peke yake.

3

Paka na Mbwa wanamwendea ndege.

Wanamwuliza, "Yai hili ni lako?"

4

Lakini ndege anasema, "La, hilo si yai langu. Mwulize bundi. Labda yai ni lake."

5

Paka na Mbwa wanamwendea bundi.

Wanamwuliza, "Yai hili ni lako?"

6

Lakini bundi anasema, "La, hilo si yai langu. Mwulize bata bukini. Labda yai ni lake."

7

Paka na Mbwa wanamwendea bata bukini.

Wanamwuliza, "Yai hili ni lako?"

8

Lakini bata bukini anasema, "La, hilo si yai langu. Waulize wale bata wawili. Labda yai ni lao."

9

Paka na Mbwa wanawaendea wale bata wawili.

Wanawauliza, "Yai hili ni lenu?"

10

Lakini wale bata wawili wanasema, "La, hilo si yai letu."

Halafu, yai linavunjika.

11

Wanamwona mjusi kwenye yai.

Mjusi mtoto.

12

Mjusi mtoto anasema, "Mama yangu yuko wapi? Baba yangu yuko wapi? Wapi baba na mama yangu?"

Paka na Mbwa wanampeleka mjusi mtoto kwa baba na mama yake.

13

Kwaheri Paka.

Kwaheri Mbwa.

Kwaheri Mjusi mtoto.

14

15
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Paka na Mbwa na Yai
Author - Elke and René Leisink
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Elke and René Leisink
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs