Mwalimu Akinyi
Lawrence A. Konjuro
Vusi Malindi

Huyu ni mwalimu wangu.

Anaitwa Mwalimu Akinyi.

Anatupenda sana.

1

Mwalimu Akinyi anatufunza alfabeti.

Anatufunza pia vokali.

Ninaweza kutaja herufi a, e, i, o, u.

2

Mwalimu Akinyi anatufunza rangi tofauti.

Ninajua rangi nyekundu, bluu, kijani, manjano, na nyeusi.

3

Tukipumzika, Mwalimu Akinyi anatuimbia.

Anatuimbia bembelezi tamu.

4

Yeye huimba hivi:

Lala watoto, lala!
Tabasamu zawangoja muamkapo.

Lala, wapenzi, msilie.
Nawaimbia bembelezi tamu.

5

Mwalimu Akinyi anajua hadithi nyingi.

Kila siku ya wiki anatusimulia hadithi tofauti.

6

Jumatatu, anatusimulia hadithi kuhusu wanaume mashujaa.

7

Jumanne, hutusimulia hadithi kuhusu wanawake mashujaa.

8

Jumatano, anatusimulia hadithi kuhusu vyombo vya usafiri.

9

Alhamisi, yeye hutusimulia hadithi kuhusu ukulima.

10

Na Ijumaa, sisi tunasimulia hadithi zetu darasani.

11

Mwalimu wetu ndiye mwalimu bora ulimwenguni!

Nitakuwa kama Mwalimu Akinyi nikiwa mkubwa.

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Mwalimu Akinyi
Author - Lawrence A. Konjuro
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Vusi Malindi
Language - Kiswahili
Level - First sentences