Nozibele na Nywele Tatu
Tessa Welch
Wiehan de Jager

Hapo zamani za kale, wasichana watatu walienda kutafuta kuni.

1

Ilikuwa siku yenye joto kwa hivyo walienda mtoni kuogelea.

Walicheza wakirushiania maji na kuogelea.

2

Ghafla, waligundua kuwa saa zilikuwa zimeenda.

Walifanya haraka kurudi kijijini.

3

Walipokuwa karibu nyumbani, Nozibele aliweka mkono wake shingoni.

Alikuwa amesahau mkufu wake! "Tafadhali rudini nami!" aliwasihi marafiki zake.

Lakini, marafiki zake walisema kwamba saa zilikuwa zimeenda sana.

4

Kwa hivyo Nozibele alirudi mtoni peke yake. Aliupata mkufu wake na kuanza kurudi nyumbani kwa haraka.

Kwa bahati mbaya, alipotea gizani.

5

Kwa umbali aliona mwangaza ukitokezea chumbani.

Alikikaribia chumba hicho na kubisha hodi mlangoni.

6

Alishangaa mbwa alipoufungua mlango na kumwuliza, "Unataka nini?"

"Nimepotea, nahitaji mahali pa kulala," Nozibele alisema.

"Ingia ndani, au nikuume!" mbwa akajibu. Nozibele aliingia.

7

Kisha mbwa akasema, "Nipikie chakula!"

"Lakini sijawahi kumpikia mbwa chakula," Nozibele aljibu.

"Pika, au nikuume!" mbwa akasema. Nozibele alimpikia mbwa chakula.

8

Tena mbwa akasema, "Nitayarishie kitanda."

Nozibele akajibu, "Sijawahi kumtayarishia mbwa kitanda."

"Tayarisha au nikuume!" mbwa alisema. Nozibele alitayarisha kitanda.

9

Alitakiwa kumpikia, kumfagilia na kumwoshea mbwa kila siku.

Siku moja mbwa alisema, "Nozibele, nimelazimika kuwatembelea marafiki zangu. Fagia nyumba, pika chakula na uoshe vitu vyangu kabla sijarudi."

10

Mbwa alipoenda tu, Nozibele alichukua nywele tatu kutoka kichwani kwake.

Aliweka mmoja mvunguni mwa kitanda, mwingine nyuma ya mlango, na mwingine kwenye zizi la ng'ombe.

Kisha alikimbia kwenda nyumbani haraka alivyoweza.

11

Mbwa aliporudi, alimwita Nozibele kwa sauti, "Uko wapi?"

"Niko mvunguni mwa kitanda," unywele wa kwanza ulisema.

"Niko nyuma ya mlango," unywele wa pili ukasema.

"Niko kwenye zizi la ng'ombe," ukasema unywele wa tatu.

12

Papo hapo mbwa alifahamu kuwa Nozibele alikuwa amemdanganya. Kwa hivyo, alikimbia moja kwa moja hadi kijijini.

Lakini, ndugu zake Nozibele walikuwa wamemsubiri kwa fimbo kubwa.

Mbwa aligeuka na kukimbia na hadi leo, hajawahi kuonekana tena.

13
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Nozibele na Nywele Tatu
Author - Tessa Welch
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Wiehan de Jager
Language - Kiswahili
Level - Longer paragraphs