Kwa nini mtoto analia?
Labda ana njaa.
Kwa nini mvulana huyu amehuzunika?
Labda anamkosa baba yake.
Kwa nini msichana huyu amefurahi?
Kwa sababu amepata rinda jipya.
Kwa nini mzee huyo anacheka?
Kwa sababu amesoma kichekesho.
Kwa nini mama huyu anatabasamu?
Kwa sababu watoto wake wanasoma kimya kimya.
Mbona mwanamke huyu anatazama chini?
Labda anaona haya.