Mwezi na kofia
Noni
Angie & Upesh

Sote tulienda katika sherehe ya Dasara.

1

Chintu alipewa miwani.

Nilipata kofia naye Moto akapata peremende.

2

Upepo mkali ulivuma.

Uliipeperusha kofia yangu mbali.

3

Kofia ilizuiliwa katika matawi ya mti wenye miiba.

4

Nililia sana.

Sikula chakula changu cha jioni.

5

Usiku mwezi ulitokezea.

Uliimulika kofia yangu pale mtini.

6

Mwezi ulijaribu kuivaa kofia yangu.

Ulitabasamu nami pia nikatabasamu.

7

Mama alinipatia kofia nyingine nyekundu.

"Mwezi uliituma," alisema.

8

Mimi na mwezi, tulivaa kofia zetu.

Tulitabasamu kwa furaha.

9

Je, jua linahitaji kofia?

10

Ni kofia gani ambayo nimevaa leo?

11
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Mwezi na kofia
Author - Noni
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Angie & Upesh
Language - Kiswahili
Level - First words