Paka mwerevu na Mbwa mjinga
Solomon Abreha
Salim Kasamba

Hapo kale, kulikuwa na Paka mwerevu na Mbwa mjinga. Paka mwerevu aliishi vizuri katika nyumba ya kifahari.

Mbwa mjinga alihisi njaa mtaani.

1

"Inawezekanaje familia tajiri kukuruhusu kuishi nyumbani kwao?" Mbwa mjinga alimwuliza yule Paka mwerevu kwa hasira.

2

Paka mwerevu alijibu, "Ninaishi na watu kwa sababu mimi ni nadhifu. Ninajua kuzika kinyesi changu. Nikihitaji chakula, mimi husema, miau."

3

"Je, mimi pia nikifanya hivyo wataniruhusu niishi
nyumbani kwao?" Mbwa akamwuliza.

Paka akajibu, "Ndiyo, fanya nilivyokueleza na watakuruhusu. Watakupatia chakula vilevile."

4

Kabla ya mazungumzo hayo, Mbwa mjinga alikuwa akitaka kumla Paka mwerevu. Baada ya mazungumzao, alisema, "Leo, sitakuumiza."

Paka aliwaza, "Lo! Nimeponea chupuchupu. Sitaki kukutana naye tena."

5

Mbwa mjinga alifuata ushauri aliopewa na Paka mwerevu.

Alikwenda nyumbani kwa tajiri akabweka kwa sauti pale mlangoni.

6

Mwenye nyumba alitoka akampiga kwa fimbo. "Huyu Paka amenidanganya. Nikimpata, nitamla." Mbwa mjinga alinung'unika.

7

Baadaye, Paka mwerevu alipokuwa akicheza nje ya nyumba, Mbwa mjinga alimwambia, "Wakati ule ulinidanganya. Nilibweke mlangoni ulivyonishauri na mwenye nyumba akanipiga. Sasa nitakula."

8

Paka mwerevu akamjibu, "Mbwa, nisikize. Ni sawa utanila. Lakini, kwanza niache nicheze. Mimi humuacha panya acheze kwanza ndivyo nimle."

9

Mbwa mjinga alimwuliza, "Panya huchezaje?" Paka akamjibu, "Mimi humwuliza ahesabu hadi tatu. Kisha humkamata anapokuwa anahesabu."

10

Basi Mbwa mjinga akamwacha Paka mwerevu huru. Kisha akamwambia ahesabu hadi tatu. Paka mwerevu alitoroka akapanda juu ya mti.

Mbwa akamwita Paka mwerevu, "Shuka, rudi hapa uhesabu hadi tatu."

11

Paka mwerevu akamjibu, "Sikiza Mbwa, hutawahi kunishika tena. Mimi si mjinga. Unaweza kuhesabu hadi mia moja, elfu au milioni, lakini hutawahi kunipata tena!"

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Paka mwerevu na Mbwa mjinga
Author - Solomon Abreha, Teki'a Gebrehiwot
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Salim Kasamba
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs