Niliwasili katika kituo chetu cha basi.
Kilikuwa kimejaa watu.
Kondakta wa basi aliita, "Kwenda jijini! Tunaondoka sasa!"
Watu walifanya haraka kuingia ndani ya basi.
Wanawake waliokuwa na watoto waliketi.
Safari itakuwa ndefu.
Niliketi kwenye dirisha karibu na mwanamume na mwanamke.
Niliwaza, "Ninaenda jijini! Nitakosa familia yangu."
Wachuuzi wengi waliingia kuuza bidhaa zao.
Baadhi ya abiria walinunua bidhaa.
Sikuwa na pesa ya kununua chochote.
Ghafla, dereva alipiga honi.
Tulikuwa tayari kuondoka.
Wachuuzi walisukumana kutoka nje.
"Tutafika saa ngapi?" Nilijiuliza.
Ndani ya basi mlikuwa na joto sana.
Niliyafumba macho yangu.
Niliwafikiri mama na ndugu yangu wakiwa nyumbani.
Baadaye, nilipatwa na usingizi.
Baada ya muda mrefu, niliamka.
Karibu kila abiria alikuwa ameshuka.
Nilianza kutafuta mahali mjomba aliishi.