Fana anawapenda wanyama
Foziya Mohammed
Jesse Breytenbach

Fana na familia yake wanaishi mjini.

1

Fana ana paka, kuku wawili, mbuzi na njiwa.

2

Siku moja Fana aliwaona watoto wakiwarushia njiwa mawe.

3

Fana alikimbia akisema, "Acheni kutupa mawe."

4

Fana aliwachukua wale njiwa akawapeleka nyumbani.

5

Aliwalisha.

Aliwaambia wazazi vile alivyowaokoa.

6

Fana na wazazi wake waliwapeleka njiwa kutibiwa.

7

Fana huwaambia wenzake, "Wanyama ni marafiki zetu. Tunawalinda."

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Fana anawapenda wanyama
Author - Foziya Mohammed
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Jesse Breytenbach
Language - Kiswahili
Level - First words