Lego alikuwa nyoka mkubwa.
Aliishi katika kijiji cha Sinyare.
Apiyo, Ajoh na Atieno walienda kutafuta kuni.
Bibi aliwaonya kuhusu Lego.
Wote watatu walitayarisha chakula.
"Itakuwa siku ndefu," walisema.
"Hebu tuwe kimya. Lego huishi karibu hapa," Apiyo aliwakumbusha dada zake.
Atieno alitaka meno ya Lego.
Apiyo alimwambia, "Kumbuka onyo la bibi."
"Ninataka meno ya Lego ya dhahabu."
Ajoh alisizitiza bila kujali.
Lego hakuyapata meno yake ya dhahabu.
Alisubiri kumwadhibu aliyeyaiba.
Wasichana walisikia sauti "Hsssss!"
Lego alikuwa tayari kumuuma aliyeiba.
Lego aliwapatia mtihani wa kuimba.
"Aliyeiba, hatafaulu kuimba vizuri."
Apiyo na Atieno waliimba vyema.
Kwa hivyo, walipita mtihani.
Ajoh hakufaulu kuimba vizuri.
Lego alijua aliyeiba meno yake ya dhahabu.
Lego alimmeza Ajoh!
Bibi aliposikia, alisema, "Heri angenisikiza."