Nilivyopotea sokoni
Timothy Kabare
Catherine Groenewald

Kijiji changu kina mbuzi.

Kiko mbali na miji mikubwa.

1

Mama aliniambia, "Tunakupa zawadi unaposherehekea miaka sita ya kuzaliwa."

2

Mimi, mama na shangazi tulisubiri basi kufika.

3

Mama alinipakata miguuni.

Nililala wakati wote tuliosafiri.

4

Tulifika sokoni.

Niliiona helikopta maridadi ya bluu.

5

Kibanda kimoja kilikuwa na matunda.

Nilimwuliza mama, "Haya yanaitwaje?"

6

Mama alijibu, "Haya ni matofaa."

"Tafadhali, ninunulie moja," nilisema.

7

Niliusahau mkona wa mama.

Nilizingatia tu lile tofaa langu.

8

Nilipomaliza kula tofaa, nilijikuta nikiwa peke yangu.

Nilianza kulia.

9

Mwanamke mmoja alinichukua.

Alinipeleka walikokuwa watoto wengine.

10

Niliwaza kuwa labda watoto waliuzwa sokoni.

Nililia zaidi.

11

Mwanamume aliuliza, "Elly yuko wapi?"

Nilijificha ili asinione.

12

Sauti ya mama niliyoijua, iliita, "Elly!"

Nilifurahi sana.

13

Shangazi yangu aliitoa helikopta maridadi.

"Ni yako!" alisema.

14
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Nilivyopotea sokoni
Author - Timothy Kabare, Ursula Nafula
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Catherine Groenewald
Language - Kiswahili
Level - First words