Kulikuwa na msichana aliyeitwa Kalabushe.
Alipenda kuongea sana.
Siku moja, shangazi yake alikuwa mgonjwa.
Aliishi peke yake.
Mama aliporudi jioni alisema, "Kalabushe, mpelekee shangazi yako chakula."
Kalabushe alikutana na fisi.
Alikuwa amebadilika kuwa mtu.
Fisi alimwuliza alichobeba.
Kalabushe alijibu, "Nyama, mayai na maziwa."
Fisi alitamani nyama. Alilamba midomo yake.
Alipanga jinsi ya kuipata.
Fisi alikimbia mbele ya Kalabushe.
Aliingia kwa shangazi akajificha.
Alimmeza shangazi kisha akajifunika blanketi lake.
Akamsubiri Kalabushe.
Kalabuse alipofika, aliita, "Shangazi, uko wapi?"
Shangazi hakumjibu.
Kalabushe alimwona mtu aliyejifunika blanketi.
Alitaka kujua.
Aliuliza, "Shangazi, mbona masikio yako ni makubwa?"
"Ili nikusikie."
Aliuliza tena, "Shangazi, mbona macho yako ni makubwa?"
"Ili nikuone."
"Shangazi, mbona mdomo wako ni mkubwa?"
Papo hapo, Fisi alimmeza.
Kalabushe aliendelea kuuliza maswali akiwa mle tumboni.
Fisi alichoshwa na maswali ya Kalabushe.
Alimtema nje.
Kalabushe na shangazi waliokolewa na wanakijiji.
Kalabushe alipata funzo.