Mamba na Mbwa
Candiru Enzikuru Mary
Rob Owen

Siku moja, Mbwa aliyapata mayai kando ya mto.

1

Mbwa aliyaweka mayai hayo kumi katika kikapu.

2

Mbwa aliyalinda na kuyaweka mahali kwenye joto.

3

Mamba alimwuliza Mbwa, "Umeyaona mayai yangu?"

4

Mamba aliwauliza wanyama wote ikiwa waliyaona mayai yake.

5

Wakati huo, mayai yaliangua moja moja.

6

Mbwa hakuweza kuwapa mamba wachanga chakula cha kutosha.

7

Siku moja, Mamba aliyasikia matumbo ya wanawe yakinguruma!

8

Mamba aliingia nyumbani akamcharaza Mbwa kwa mkia wake.

9

Mamba alimkimbiza Mbwa barabarani.

10

Mbwa alisimama akamwambia Mamba, “Nisamehe!”

11

Mamba alimsamehe. Alienda na wanawe kuogelea.

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Mamba na Mbwa
Author - Candiru Enzikuru Mary
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Rob Owen
Language - Kiswahili
Level - First words