Bibi, Sungura na Tembo
Mutai Chepkoech
Marleen Visser

Bibi alianza, “Sungura na Tembo walikuwa marafiki tena majirani.”

1

Sungura alipenda uyoga lakini alikuwa mvivu sana. Hakulima.

2

Sungura hakupata uyoga.

Alianza kuiba ndizi za Tembo.

3

Tembo aliimba, “Nitamshika mwizi!”

Sungura aliogopa.

4

Kima alimchungia Tembo shamba lake.

Lakini, Sungura hakuiba.

5

Tembo alienda kutazama.

Sungura alijificha ndani ya matawi ya maboga.

6

Tembo aliangalia kila mahali.

Hakumpata mwizi.

7

Siku nyingine, Sungura alijificha ndani ya boga kubwa.

8

Tembo aliliona hilo boga kubwa akalimeza.

9

Boga lilisonga tumboni mwa Tembo.

10

Tembo alilitema boga.

Sungura alitoka ndani akatoroka.

11

Bibi alisema, “Na huo ndio mwisho wa hadithi.”

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Bibi, Sungura na Tembo
Author - Mutai Chepkoech
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Marleen Visser
Language - Kiswahili
Level - First words