Hapo zamani, paka na panya walikuwa marafiki.
Panya walianza kupoteza baadhi ya jamaa zao.
Panya mmoja mzee alisema, "Nadhani paka wanatula."
Akina mama waliwaambia watoto wao, "Kueni waangalifu. Msiende nje."
Panya wote walikuwa waangalifu.
Waliketi ndani ya mashimo yao.
Paka walianza kuwa na njaa.
Waliuliza, "Panya wako wapi?"
Paka waliwatembelea panya.
Walitaka kupanga harusi kati yao.
Walisema, "Tungependa binti wenu mmoja aolewe kwa mvulana wetu."
Panya waliwaambia paka, "Mnadanganya. Mnataka kutula."
Mwishowe, walikubali kuwa na harusi kati ya wanao.
Paka walirudi nyumbani kwa furaha.
Walilamba midomo yao.
Siku ya harusi, panya walikuwa waangalifu sana.
Paka waliwasili wakiimba wimbo wa harusi.
Wimbo ulisema, "Washikeni muwale."
Panya mzee alianza kuimba, "Kimbieni, panya, kimbieni."
Panya mzee aliwaambia paka, "Sisi nanyi si marafiki."