Jumamosi moja
Nombulelo Thabane
Wiehan de Jager

Jumamosi moja, mama alisema, "Brenda, Maria na Lona, nendeni mcheze!"

Waliondoka mbio pamoja.

1

Lona alisema, "Twendeni mtoni tukaogelee."

Brenda alijibu, "Mama alitukataza kuogelea mtoni."

2

Walifika mtoni wakavua viatu na nguo.

Wakacheza majini kwa muda.

3

Walicheka na kushangilia.

Walifurahia maji baridi.

4

Baadaye, Maria alisema, "Tuogelee zaidi. Mama hatajua."

Lona na Brenda walikubali wakaendelea kuogelea.

5

Walipomaliza, hawakuziona nguo zao popote.

Walianza kuhisi baridi.

6

Hawakuzipata nguo zao popote.

"Tutamwambia mama nini?" Waliulizana.

7

Brenda alisema, "Lo! Ng'ombe anakula shati la Lona."

Lona alianza kulia.

8

"Mwingine anakula sketi yangu!" Maria pia alilia.

9

Walisema, "Mama, ng'ombe walikula nguo zetu."

Hawakusahau adhabu aliyowapa.

10

Maswali: 1.Taja majina ya watoto wote watatu tunaokutana nao katika hadithi hii. 2. Kwa mujibu wa Brenda, Mama aliwakataza watoto kufanya nini? 3. Watoto walihisije walipomaliza kuogelea? 4. Unafikiri watoto hawa walikuwa wamewahi kuogelea katika mto huo? Toa sababu kwa jibu lako. 5. Unafikiri watoto hawa walipewa adhabu gani?

11
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Jumamosi moja
Author - Nombulelo Thabane, Tessa Welch
Adaptation - Ursula Nafula
Illustration - Wiehan de Jager
Language - Kiswahili
Level - First sentences