Sungura amdanganya Tembo
Agnes Gichaba
Wiehan de Jager

Tembo na Sungura walikuwa marafiki.

1

Walilisha mifugo yao sehemu iliyokuwa na nyasi na maji.

2

Walizoea kucheza mpira wa miguu.

3

Tembo alifunga mabao mengi.

Sungura hakufurahi.

4

Sungura aliuliza, "Nini inakusaidia kucheza vyema?"

"Miguu yangu minono."

5

Sungura na Tembo walishindana mbio.

Sungura alishinda.

6

Alimwuliza, "Nini inakusaidia kwenda mbio?"

"Miguu yangu myembamba."

7

Tembo alimwuliza Sungura, "Nitapataje miguu myembamba?"

"Nitakuonyesha."

8

Sungura alisema, "Simama ndani ya moto." 

Tembo alilia, "Ninaungua!"

9

Sungura alisema, "Hii ndiyo njia pekee ya kuipata miguu  myembamba."

10

Tembo alilala chini.

11

Kwa siku nyingi, hakuweza kusimama.

12

Alipopata nafuu, alienda nyumbani kwa familia yake.

13

Sungura alisikitika sana.

Alimwomba Tembo msamaha.

14
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Sungura amdanganya Tembo
Author - Agnes Gichaba
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Wiehan de Jager
Language - Kiswahili
Level - First words