Kwa nini viboko hawana manyoya
Basilio Gimo
Carol Liddiment

Siku moja, Sungura alikuwa anatembea ukingoni mwa mto.

1

Kiboko alikuwa akila majani matamu ya kijani.

2

Kwa bahati mbaya, Kiboko alimkanyaga Sungura mguuni.

Kwa uchungu, Sungura alipiga mayowe  na kumfokea Kiboko akisema, "Wewe Kiboko! Unaukanyaga mguu wangu. Huoni?"

3

Kiboko alimuomba Sungura msamaha, "Samahani sana rafiki. Sikukusudia. Naomba unisamehe!"

Sungura hakumsikiliza. Aliendelea kumfokea Kiboko akisema, "Umefanya makusudi! Siku moja nitalipiza kisasi!"

4

Siku moja, Sungura alimtafuta Moto na kumwambia, "Naomba umuunguze Kiboko atakapotoka kwenye maji baada ya kula majani. Kanikanyaga!"

Moto akajibu, "Hapana shaka, rafiki yangu Sungura. Nitafanya ulivyoniambia."

5

Kiboko alipokuwa akila majani kando ya mto, "Whuuush!" Moto akalipuka na kuanza kuyaunguza manyoya ya Kiboko.

6

Kiboko alilia kwa uchungu huku akikimbilia majini. Manyoya yake yote yaliungua. 

Kiboko alipiga mayowe, "Manyoya yangu yameunguzwa! Moto ameyaunguza manyoya yangu yote! Manyoya yangu yameungua! Manyoya yangu mazuri!"

7

Tangu wakati huo, kiboko hatembei mbali na maji kwa kuhofia kuunguzwa na Moto.

Sungura alifurahi sana kumuona Kiboko bila manyoya. Akasema, "Nimelipiza kisasi!"

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Kwa nini viboko hawana manyoya
Author - Basilio Gimo, David Ker
Translation - Wilkins Kiondo
Illustration - Carol Liddiment, Little Zebra Books
Language - Kiswahili
Level - Longer paragraphs