Lodipo amtoroka mama
John Nga'sike
Zablon Alex Nguku

Hapo zamani za kale, paliishi mzee aliyeitwa Lodipo.

Aliishi na wakeze wawili, Akila na Akitela.

1

Mamake Lodipo alikuwa kipofu.

Akitela pekee ndiye aliyekuwa akimsadia.

2

Siku moja, Akila alimwambia Lodipo, "Tuondoke kijijini humu twende kuliko na amani."

Kijijini mwao kulikuwa na uvamizi wa mara kwa mara.

3

Lodipo akamwambia Akila kuwa hawangeweza kumuacha mama yake pekee. Akila alisisitiza waondoke na wamuache ajuza huyo.

"Kama wewe hutaki kuondoka hapa, mimi nitarudi kwa wazazi wangu," Akila alimfokea Lodipo.

4

Lodipo alimpenda sana Akila. Hivyo, alikubaliana naye na kupanga watakavyotoroka.

Akitela alishangazwa na haya yote.

5

Siku moja, mamake Lodipo alikuwa ameketi chini ya mti. Hakufahamu kilichokuwa kikiendelea.

Huku akimwangalia na kumhurumia, Akitela alitafakari, "Itakuwaje tukimwacha peke yake?"

6

Lodipo na wakeze wawili walipakia mizigo yao kwenye ngamia wao wawili. Wakaondoka kimya kimya bila kumuaga yule ajuza.

Akitela alikuwa akilia kwa huzuni ya kumuacha mama mkwe. Aliwaza, "Nitajificha nirudi kuwa naye."

7

Ajuza huyo alipoachwa peke yake nyumbani, alilia na kuimba wimbo huku akimtaja Lodipo.

8

Punde, Lodipo na wakeze wawili walipoondoka, wezi wa mifugo walivamia kijiji.

9

Wezi hao walimwambia ajuza awaeleze alikokwenda mwanawe.

Majambazi hao walimwambia kuwa wangemtafuta Lodipo wamuadhibu.

Ajuza aliwaomba majambazi wasimdhuru Akitela.

10

Pia aliwaambia wamrudishie kondoo dume aliyekuwa amechukuliwa na Lodipo.

11

Majambazi walimtafuta Lodipo na kumpata katika kijiji kipya.

Walimshambulia Lodipo na Akila, mkewe wa pili.

12

Akitela alirudi kijijini pamoja na yule kondoo dume wakaishi kwa furaha.

13
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Lodipo amtoroka mama
Author - John Nga'sike
Translation - Ramadhan Rajab
Illustration - Zablon Alex Nguku
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs