Nausikiliza mwili wangu
Noni
Angie & Upesh

Leo ni likizo!

Siendi shule.

1

Leo hakuna umeme.

Sitatazama runinga.

2

Nitafanya nini leo?

Nitausikiliza mwili wangu!

3

Ili niweze kuusikiliza mwili wangu, lazima niwe kimya.

Kimya kabisa.

4

Sasa naweza kuisikia pumzi yangu.

Pumua. Toa.

Pumua. Toa.

5

Ninaweza kufanya pumzi yangu isikike kwa sauti ya juu. Zzzzzzzzz!

Au isikike kwa sauti ya chini. Mhmhmhmh.

6

Sasa nausikia moyo wangu ukidunda! Kudukudukudu.

7

Je, naweza kuufanya moyo wangu kwenda mbio au kudunda kwa sauti ya juu?

Ndiyo, nikiruka juu na chini mara nyingi.

8

Sasa moyo wangu unadunda kwa kasi.

Dudududu!

9

Nikiweka kidole changu mkononi nitaweza kuusikia mpigo wa moyo wangu!

10

Ninajisikia nikicheka.

Haha haha haaah haaa!

11

Ninajisikia nikilia.

Boohoooohooo!

12

Ninasikia nikipiga makofi.

Pa papa papapa papapapa.

13

Ninaweza kulisikia tumbo langu likinguruma.

Gururuuuuu.

14

Likisema, nilishe, nilishe.

15

Na mapua yangu yananusa keki ipikwayo jikoni na mama.

16

Kuusikiliza mwili wangu, ni jambo la kufurahisha.

Sasa nataka kuzisikiliza taya zangu zikitafuna.

17

Na tumbo langu likifurahia keki tamu zilizookwa na mamangu!

18
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Nausikiliza mwili wangu
Author - Noni
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Angie & Upesh
Language - Kiswahili
Level - First sentences