Msitu wenye nyoka
Joseph Sanchez Nadimo
Rob Owen

Kijiji cha Sinyaire kimezungukwa na milima na misitu. Nyoka wengi huishi ndani ya misitu hiyo.

Wanakijiji walimwita Unyalego nyoka aliyekuwa mkubwa zaidi. Nyoka huyo aliwameza mbuzi na kondoo wakiwa wazima.

1

Siku moja, Apiyo, Ajoh na Atieno walienda msituni kutafuta kuni.

Bibi aliwaonya, "Jihadharini na Unyalego. Msichukue chochote kutoka msituni ila kuni."

2

Wasichana hao walifunganya maziwa, ndizi, viazi vitamu na maji.

Wakachukua kamba za kufungia kuni na panga kali.

Wakaondoka kwenda msituni.

3

Walipokuwa njiani, Ajoh, Apiyo na Atieno waliongea na kucheka.

Ghafla, Apiyo alisema, "Kimya! Tunakaribia anakoishi Unyalego."

4

Ajoh hakuzingatia onyo la bibi. Atieno aliwaita, "Tazameni, hapa kuna meno ya Unyalego ya dhahabu. Tuyachukue?"

Apiyo aliwakumbusha, "Msisahau kwamba bibi alituonya tusichukue chochote kutoka msituni ila kuni."

5

Ajoh akajibu, "Simwamini bibi. Nadhani alisema hivyo ili atuzuie kuchukua tunachotaka. Najua anatuonea wivu. Mimi nitayachukua hayo meno ya dhahabu."

Dada zake walikuwa na wasiwasi wakamwonya Ajoh lakini, hakujali.

6

Baadaye, Unyalego alikuja kutafuta meno yake. Alikasirika alipoyakosa.

Aliwasikia Ajoh, Apiyo na Atieno wakizungumza na kucheka.

Akajificha kando ya njia ambayo wasichana wale wangepitia.

7

Walipokwisha kuzikusnaya kuni, walizibeba vichwani. Ghafla, wakasikia "Hzzzzzzzzz!"

Walimwona Unyalego akiwa kinywa wazi, tayari kuwameza. Waliogopa sana wakajaribu kujificha.

8

Unyalego akawauliza, "Ni nani aliyeyachukua meno yangu ya dhahabu?" Walipokosa kumjibu, Unyalego akaamua kuwadadisi wasichana hao.

Akasema, "Ninataka muimbe wimbo. Yule atakayeimba bila kukosea, atakuwa hana hatia na ataenda nyumbani na kuni zake. Atakayekosea, ndiye aliye na hatia na atakuwa chakula changu kwa siku tatu zijazo!"

9

Apiyo aliimba kwanza kwa sauti nyororo:

Sio mimi, sio mimi niliyeiba meno, aliyeyaiba yuko hapo nyuma aaaah.

Kisha Atieno akaimba:

Sio mimi, sio mimi niliyeiba meno, aliyeyaiba yuko hapo nyuma aaaah.

10

Mwishowe, ilikuwa zamu ya Ajoh. Kwa uwoga alisongea mbele na kuanza kuimba:

S.i.o mi-mi, s.i.o. 

Aliimba vibaya akashindwa kuyatamka maneno sawa. Unyalego akamkemea, "Mbona huimbi vizuri kama wengine?"

11

Papo hapo, Unyalego akammeza Ajoh. 

Atieno na Apiyo walikimbia kuwaeleza wanakijiji yaliyotokea.

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Msitu wenye nyoka
Author - Joseph Sanchez Nadimo
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Rob Owen
Language - Kiswahili
Level - Longer paragraphs