Sungura na Tembo (Tena!)
Agnes Gichaba
Wiehan de Jager

Hapo zamani za kale, Tembo na Sungura walikuwa marafiki wakubwa sana.

Walikuwa na ngamia, ng'ombe na kondoo wengi.

1

Waliwalisha wanyama hao katika bonde la Kingilo.

Wakati mwingine waliwapeleka milimani kulikokuwa na nyasi na maji kwa wingi.

2

Wanyama walipokula, Sungura na Tembo walicheza.

Walipenda sana kucheza mpira wa miguu.

3

Kila walipocheza, Tembo aliingiza goli nyingi kumliko Sungura.

Sungura alikasirishwa mno na hali hiyo.

4

Siku moja Sungura alimwuliza Tembo, "Ni nini kinachokuwezesha kuwa mwingizaji goli maarufu?"

Tembo alimjibu, "Ni miguu yangu minono."

5

Siku iliyofuata, Sungura alipendekeza wawe na mashindano ya mbio.

Tembo alikubali na wakaanza mbio.

6

Sungura alishinda mbio zote. Tembo alikasirika. Hakuwahi kushindwa.

Alimwuliza Sungura, "Ni nini kinachokuwezesha kuwa mkimbiaji maarufu?" 

Sungura alijibu, "Ni miguu yangu myembamba."

7

Tembo alimwuliza, "Nitawezaje kupata miguu myembamba?"

Sungura akamjibu, "Ni rahisi, nitakuonyesha. Tafuta kuni ukakoke moto."

8

Tembo alizikusanya kuni akakoka moto mkubwa. Sungura akamwambia, "Sasa iweke miguu yako ndani ya moto."

Tembo alifanya hivyo. Alipiga kelele, "Ninaungua! Ninaungua!"

9

Sungura alifurahi. Alimhimiza Tembo aendelea hivyo hivyo.

Alisema kuwa hivyo tu ndivyo miguu yake ingekuwa myembamba.

10

Miguu ya Tembo ilijeruhiwa vibaya akaondoka motoni.

Hakuweza kusimama kwa hivyo alilala chini.

11

Tembo aliketi kwa siku nyingi kabla kuweza kusimama.

12

Hatimaye, aliweza kuchechemea na kwenda nyumbani kwa familia yake.

13

Sungura alimwomba Tembo msamaha.

Hata hivyo, urafiki kati ya Tembo na Sungura uliisha.

14
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Sungura na Tembo (Tena!)
Author - Agnes Gichaba
Illustration - Wiehan de Jager
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs