Mlinzi na chekechea yake
Ursula Nafula
Magriet Brink

Hadithi hii anamhusu Mlinzi na chekechea yake ya wanyama mayatima.

1

Agosti ulikuwa mwezi wenye shughuli nyingi.

Mlinzi na wasaidizi wake waliwapokea wanyama wengi katika chekechea yao.

2

Mkite alikuwa wa kwanza kufika.

Alikuwa mtoto wa tembo mwenye umri wa mwaka mmoja.

3

Mlinzi na wasaidizi wake walimhurumia Mkite sana.

Alikuwa amekonda na mwenye huzuni.

4

Siku chache baadaye, afya ya Mkite iliimarika. 

Alicheza na wanyama wengine aliowakuta pale.

5

Siku nyingine katika mwezi huo wa Agosti, helikopta ilitua mbele ya chekechea.

6

Walimpokea yatima wa pili katika mwezi huo.

Alikuwa mtoto mwingine wa tembo. Alifunikwa kwa blanketi.

7

Yatima huyo aliitwa Ndiwa. Alikuwa na umri wa siku tano.

Mlinzi alimnywesha maziwa kwa kutumia chupa.

8

Yatima wa tatu kufika mwezi huo alikuwa Malea, kifaru.

Malea alikwa na umri wa miezi sita.

9

Enkare alikuwa nyati mtoto. Yeye na Malea walikuwa marafiki wakubwa.

Walienda kila mahali pamoja.

10

Usiku mmoja, Mlinzi na wasaidizi wake waliamshwa.

Walimpokea twiga mtoto waliyemwita Ambia.

11

Ambia alikuwa na umri wa miezi mitano.

Alihisi njaa na uchovu baada ya safari ndefu.

12

Kwa sababu ya urefu wake, Mlinzi aliupanda mti kumlisha.

13

Abei na Moit, swara mapacha, walifika katikati ya mwezi wa Agosti.

Walikuwa wamezaliwa saa chache tu na walikuwa wagonjwa sana.

14

Walihuzunika Abei alipoaga dunia wiki moja baadaye. 

Mlinzi na wasaidizi wake walimwokoa Moit.

15

Mayatima wa mwisho kufika mwezi huo wa Agosti walikuwa Kopi, Kepi na Keji.

Walikuwa wana wa simba wenye umri wa wiki mbili. Walikuwa na kiu sana.

16

Mlinzi na wasaidizi wake waliwapenda wanyama wote hata wale watukutu.

17

Mtukutu kwa wote alikuwa Lobolia.

Alizoea kuichukua miwani ya Mlinzi.

18

Wafanyakazi wa chekechea wanafanya bidii kuwatunza wanyama hao.

Watakapoweza kujitegemea, watarudi porini.

19

MAZOEZI:   Soma tena hadithi kisha ujibu maswali haya. 1. Wanyama wangapi walifika katika chekechea mwezi Agosti? 2. Nani alifika kwanza? 3. Mnyama huyu alikuwa na umri gani? 4. Nani alifika mwisho? Wanyama hao walikuwa na umri gani? 5. Wanyama gani waliokuwa na umri wa chini zaidi? 6. Walikuwa na umri gani? 7. Mnyama yupi aliyefika mwezi Agosti aliyekuwa mzee kwa wote?

20
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Mlinzi na chekechea yake
Author - Ursula Nafula, Nina Orange
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Magriet Brink
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs