Ah! Mpira!
Stella Kihweo
Onesmus Kakungi

Mimi ninapenda kucheza na rafiki yangu Chuma.

1

Mimi na Chuma tunapendana sana.

Tukitumwa, tunaenda pamoja.

2

Siku moja nilitumwa na bibi dukani nikanunue chumvi na mafuta.

Nilienda na Chuma.

3

Tukiwa njiani, tuliwaona watoto wenzetu wakicheza mpira wa miguu.

4

Mimi nilitamani sana kucheza mpira huo.

Nilisema, "Ah! Mpira!"

5

Nilimwambia Chuma, "Twende tuwaombe kucheza nao mpira. Mimi hupenda mpira wa miguu."

6

Chuma alinijibu, "Twende kwanza dukani, halafu turudi kucheza."

7

Lakini, nilimwambia Chuma, "Tucheze kwanza wewe! Tukienda nyumbani bibi hataturuhusu."

8

Tulikubaliwa na wenzetu tukacheza mpira.

Nilikuwa golikipa.

9

Nilijitahidi kudaka mpira.

Wenzangu hawakuweza kufunga goli hata moja.

10

Uwanja tuliochezea ulikuwa na mchanga mwingi.

Magoli yake yalikuwa mawe makubwa.

11

Baada ya mchezo, tuliondoka kwenda dukani, lakini, hatukuwa na pesa. Nilianza kulia.

Chuma alinikemea, "Acha kulia. Ni wewe ulitaka tucheze kabla ya kwenda dukani."

12

Tulirudi nyumbani bila chumvi wala mafuta.

Pia, tulikuwa tumechafuka kweli kweli.

13

Tulimkuta bibi amekasirika mno.

Alituuliza, "Mmekuwa wapi muda huu wote?"

14

Alipogundua kuwa tulipoteza hela, alisema, "Nawasamehe leo, lakini, msirudie tena kucheza bila ruhusa."

15

Tulipoona tumesamehewa, tulienda haraka kuwalisha kuku na bata.

Baadaye, tulioga na kuwa wasafi.

16
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Ah! Mpira!
Author - Stella Kihweo
Illustration - Onesmus Kakungi
Language - Kiswahili
Level - First sentences