Nguruwe hawaruhusiwi
Basilio Gimo
Little Zebra Books

Miaka mingi iliyopita, jamii ya wanyama wenye pembe iliamua kuandaa karamu kubwa milimani.

Wanyama wote wenye pembe walialikwa.

1

Nguruwe aliposikia kuhusu karamu hiyo, aliwaza, "Mimi sina pembe. Je, nitafanyaje ili nihudhurie karamu hiyo?"

2

Nguruwe aliamua lazima angeshiriki katika ile karamu.

Alisonga pembe kwa kutumia nta na kuzipachika kichwani mwake!

3

Nguruwe alifaulu na akakubaliwa kuhudhuria karamu hiyo.

Karamu iliandaliwa juu milimani karibu na jua.

4

Karamu ilipokuwa ikiendelea, joto lilizidi na nta ikaanza kuyeyuka. Mara pembe za nguruwe zikaanguka chini pu!

Wanyama walipomwona nguruwe bila  pembe walishangaa na kuulizana, "Ni nani yule asiye na pembe? Kwa nini alialikwa?"

5

Mfalme wa wanyama aliamuru nguruwe ainuliwe juu na kisha aangushwe.

Walimnyanyua nguruwe na kumtupa chini kwenye bonde kubwa.

6

Maskini nguruwe, aliangukia pua lake.

Papo hapo, pua lake likabadilika na kuwa refu kama linavyoonekana hadi sasa.

7

Usishangae unapoliona pua la nguruwe jinsi lilivyo.

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Nguruwe hawaruhusiwi
Author - Basilio Gimo
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Little Zebra Books
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs