Piga hatua uoshe!
Jean de Dieu Bavugempore
Rob Owen

Mama, Baba na Lina wanaongea kuhusu kukaa katika hali nzuri ya kiafya.

1

Lina aliuliza shuleni, "Kwa nini tuioshe mikono yetu?"

2

Mwalimu alisema, "Mikono yetu ina viini, lakini hamwezi kuviona."

3

"Viini ni viumbe vidogo sana. Tunahitaji darubini kuviona."

4

Lina alitazama kwenye darubini.

Aliviona viini vilivyotoka mkono wake.

5

"Virusi na bakteria ni viini.

Viini vinaweza kutuambukiza ugonjwa."

6

"Kuosha mikono kunaweza kuzuia virusi na bakteria kuenea," Mwalimu anasema.

7

Baba anatengeneza kifaa cha kuosha mikona bila mfereji.

8

Lina anauliza, "Kifaa hiki kinatumikaje?"

9

"Kipande cha mbao kinainamisha mtungi kisha maji yanamwagika nje."

10

"Osha kwa sabuni na maji. Polepole, hesabu hadi 20 unapoosha."

11

"Baba, wewe mwerevu! Sasa, unaweza kuwasalimu watu kutumia kiwiko chako?"

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Piga hatua uoshe!
Author - Jean de Dieu Bavugempore
Adaptation - African Storybook
Illustration - Rob Owen
Language - Kiswahili
Level - First words