Adhabu
Adelheid Marie Bwire
Melany Pietersen

Siku moja, mamangu alinunua matunda aina tofauti.

1

Tulijiuliza, "Mama atatugawia matunda wakati gani?"

2

Baadaye, kakangu, Rahim, alijificha na kuyala matunda yote!

3

Tulisema kwa hasira, "Rahim ni mtukutu tena ni mchoyo. Lazima aadhibiwe."

4

Mama aligundua kuwa matunda yote yalikuwa yameliwa.

Alikasirika sana.

5

Tulimtazama Rahim kwa ukali.

6

Nilimwuliza mama, "Je, utamwadhibu Rahim?"

7

Baadaye, Rahim alipata adhabu asiyoitarajia.

8

Hakuweza kutulia!

9

Mama alipomwuliza alijibu kwa sauti ya chini, "Naumwa na tumbo."

10

Hiyo ilikuwa adhabu mbaya kuliko kama Rahim angechapwa na mama.

11

Alipopata nafuu, Rahim alituomba msamaha.

Aliahidi kuwa hataiba tena.

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Adhabu
Author - Adelheid Marie Bwire
Illustration - Melany Pietersen
Language - Kiswahili
Level - First words