Simbi ampata mama mpya
Rukia Nantale
Benjamin Mitchley

Mama yake Simbi aliaga dunia.

Simbi na baba yake walisaidiana.

1

Siku moja, baba yake Simbi alikwenda nyumbani na mwanamke.

Aliitwa Anita.

2

Baba yake alimtaka Simbi kumkubali Anita kama mama yake.

3

Simbi hakufurahi.

Alipata faraja kwa kulishika blanketi la mama yake.

4

Baba yake Simbi alienda kufanya kazi mbali. 

Anita na Simbi hawakufurahi.

5

Anita alizoea kumpiga Simbi.

Wakati mwingine, alimnyima chakula.

6

Anita alimvuta Simbi kutoka kitandani.

Blanketi la mama yake liliraruka.

7

Simbi alitoroka nyumbani.

Alilibeba lile blanketi pamoja na chakula.

8

Alipanda akaketi juu ya mti.

Alimwimbia mama yake wimbo.

9

Mwanamke mmoja aliusikiliza wimbo huo kwa makini.

10

Alifahamu kuwa Simbi ni mtoto wa ndugu yake.

11

Simbi alienda na shangazi yake.

Alikula na kulala vizuri.

12

Baba aliporudi nyumbani, hakumkuta Simbi.

13

"Unaweza kuishi na shangazi yako wakati wowote unapotaka." Baba alisema.

14

Anita na Simbi walianza kupendana.

15

Anita aliwapikia chakula.

Simbi alijua angerudi nyumbani wakati wowote.

16
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Simbi ampata mama mpya
Author - Rukia Nantale
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Benjamin Mitchley
Language - Kiswahili
Level - First words