Magozwe apata makao mapya
Lesley Koyi
Magriet Brink

Kulikuwa na wavulana wa kurandaranda mtaani.

Mdogo wao aliitwa Magozwe.

1

Alipokuwa na umri wa miaka mitano, wazazi wake walikufa.

Magozwe alienda kuishi na Mjomba Bunu.

2

Mjomba Bunu alikuwa mtu mbaya.

Magozwe alitoroka akaanza kuishi mtaani.

3

Maisha mtaani yalikuwa magumu.

Magozwe na wenzake waliomba kutoka kwa watu.

4

Siku moja, Magozwe aliokota kitabu cha hadithi kwenye pipa.

5

Kitabu kilikuwa na picha za rubani.

Magozwe alitamani kuwa rubani mashuhuri.

6

Wakati mmoja, Magozwe alikutana na Tomaso.

7

Tomaso alimpeleka Magozwe na wenzake pahali pa kupata chakula.

8

Tomaso alimwuliza Magozwe asome kile kitabu.

Magozwe alimjibu, "Sijui kusoma."

9

Magozwe pia alimweleza Tomaso, "Nilitoroka nyumbani kwa Mjomba Bunu. Yeye alikuwa mtu mbaya."

10

"Ungependa kujua kusoma?" Tomaso alimwuliza Magozwe.

Tomaso alimpatia kitabu kipya cha hadithi.

11

Magozwe alifikiria juu ya kwenda shule.

Mjomba Bunu aliwahi kumwambia, "Wewe ni mjinga. Hujui chochote."

12

Magozwe alipokumbuka maneno ya mjombake, aliogopa.

Tomaso alimwambia, "Usiogope. Wewe si mjinga."

13

Tomaso alimpeleka Magozwe na wavulana wengine katika makao ya watoto.

Walifurahi sana.

14

Magozwe alianza kwenda shuleni.

Alipenda kuwa shuleni. Alisoma kwa bidii.

15

Siku moja, Magozwe alimweleza Tomaso, "Nitakuwa rubani maarufu kuliko wote."

16

MASWALI: 1. Kwa nini Magozwe aliishi mtaani? 2. Nini ilimhamasisha Mazogwe kuwa rubani wa ndege? 3. Vitendo vipi vya Tomaso vilionyesha upendo wake kwa watoto? 4. Unafikiri Magozwe atatimiza ndoto yake ya kuwa rubani maarufu? Toa sababu tatu kwa jibu lako.

17
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Magozwe apata makao mapya
Author - Lesley Koyi
Adaptation - Ursula Nafula
Illustration - Magriet Brink, Wiehan de Jager
Language - Kiswahili
Level - First sentences