Magozwe
Lesley Koyi
Wiehan de Jager

Kulikuwa na wavulana wa kurandaranda mtaani.

Mdogo wao aliitwa Magozwe.

1

Wazazi wa Magozwe walikufa akiwa mdogo.

Alienda kuishi na mjombake.

2

Mjombake alimtesa.

Magozwe alitorokea mtaani.

3

Maisha ya mtaa yalikuwa magumu.

Waliishi kwa kuombaomba.

4

Siku moja, Magozwe aliokota kitabu cha hadithi kwenye pipa la takataka.

5

Picha zilionyesha rubani.

Magozwe alitamani kuwa rubani mashuhuri.

6

Magozwe alikuwa akiomba chakula barabarani.

Alikutana na Tomaso.

7

Tomaso aliwapeleka pahali walikopata chakula.

8

Siku moja, Magozwe alimwambia Tomaso, "Sijui kusoma."

9

Magozwe pia alimweleza kwa nini alitoroka kwa mjombake.

10

Magozwe alisherehekea miaka kumi ya kuzaliwa.

Tomaso alimpatia kitabu.

11

Magozwe alifikiria juu ya kwenda shule.

12

Ingawa aliogopa, Tomaso alimtia moyo.

13

Magozwe alipelekwa katika makao ya watoto.

14

Alisoma kwa bidii.

15

Siku moja, Magozwe alimweleza Tomaso, "Nitakuwa rubani maarufu kwa wote."

16
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Magozwe
Author - Lesley Koyi
Adaptation - Ursula Nafula
Illustration - Wiehan de Jager
Language - Kiswahili
Level - First words