Khalai anapenda mimea
Ursula Nafula
Jesse Pietersen

Khalai ni msichana mwenye umri wa miaka saba.

Katika jamii yake, jina lake lina maana sawa na 'aliye mzuri'.

1

Khalai anaamka na kuuzungumzia mmea mchanga wa Mchungwa.

Anasema, "Tafadhali Mchungwa, kua mkubwa uzae machungwa mengi mabivu."

2

Khalai anapokuwa njiani kwenda shuleni, anazizungumzia Nyasi.

Anasema, "Tafadhali Nyasi, zidi kuwa kijani kibichi na wala usinyauke."

3

Khalai anayapita Maua ya kichakani

Anasema, "Tafadhali Maua, endelea kunawiri ili nikutumie kuzirembesha nywele zangu."

4

Anapokuwa shuleni, Khalai anauzungumzia Mti ulioko pale shuleni.

"Tafadhali Mti, yazae matawi makubwa ili tuweze kusomea chini ya kivuli chako."

5

Khalai anauzungumzia Ua unaoizingira shule yake.

"Tafadhali Ua, kua uwe mwenye nguvu ili uilinde shule yetu dhidi ya watu wabaya."

6

Anaporudi nyumbani alasiri, Khalai anautembelea mti wa mchungwa kutazama ikiwa machungwa yameiva.

7

"Machungwa bado mabichi," Khalai anashusha pumzi.

"Nitakutembelea kesho, Mchungwa wee! Labda utanipa chungwa mbivu wakati huo."

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Khalai anapenda mimea
Author - Ursula Nafula
Illustration - Jesse Pietersen
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs