Khalai ni msichana mwenye umri wa miaka saba.
Katika jamii yake, jina lake lina maana sawa na 'aliye mzuri'.
Khalai anaamka na kuuzungumzia mmea mchanga wa Mchungwa.
Anasema, "Tafadhali Mchungwa, kua mkubwa uzae machungwa mengi mabivu."
Khalai anapokuwa njiani kwenda shuleni, anazizungumzia Nyasi.
Anasema, "Tafadhali Nyasi, zidi kuwa kijani kibichi na wala usinyauke."
Khalai anayapita Maua ya kichakani
Anasema, "Tafadhali Maua, endelea kunawiri ili nikutumie kuzirembesha nywele zangu."
Anapokuwa shuleni, Khalai anauzungumzia Mti ulioko pale shuleni.
"Tafadhali Mti, yazae matawi makubwa ili tuweze kusomea chini ya kivuli chako."
Khalai anauzungumzia Ua unaoizingira shule yake.
"Tafadhali Ua, kua uwe mwenye nguvu ili uilinde shule yetu dhidi ya watu wabaya."
Anaporudi nyumbani alasiri, Khalai anautembelea mti wa mchungwa kutazama ikiwa machungwa yameiva.
"Machungwa bado mabichi," Khalai anashusha pumzi.
"Nitakutembelea kesho, Mchungwa wee! Labda utanipa chungwa mbivu wakati huo."